Kelvin Kimani

LAITI

Shairi

Si huku, si huko – wapi sikuranda, nikayumba…

Lipi sikutenda – kwa wingi  wa mashobo

Na kichwa kigumu na sikio lisilosikia dawa

Wala la mwadhini

Mama kasema lipi? Mwalimu je?

Sayari ya athi  ikanipeleka chuo

Chuo kilichokosa mwelekeo – kikanipepesa na kunirusha ovyo.

Na baba…

Laiti angalikuwa hai,

Angalinionyesha tariki,

Angaliniambia ukweli,

Ukweli ninaougundua kwa uchungu mwingi.

Kuwa mtima, mdanganyifu – nisiuamini katu.

Kuwa maisha mlima, nisiyaparamie kwa pupa

Pupa ambayo imenitongoza kupenda

Visivyotamanika.

Ningalipunguza  uguo la moyo

Fundo chungu lililokatalia kooni, limekaa sawia

Nisingaliweka ya chemba wazi, penye fisi

Wanaobeua na wingi bughudha

Angaliniambia, ‘mwanangu nakupenda’

Hilo lingenipa mtizamo.

Ningalijua pakuelekea, pakuegemea hata pakuepuka

Nisingalikuwa nalia sasa hivi

Nisingalichafua hiki kitabu kwa machozi na wino

Humu gizani, giza totoro la jela.

Written on July 4, 2017 and first draft appeared on poetryfolks